Thursday, 1 November 2012

Apple ordered to re-write 'inaccurate' Samsung statement

Apple has 48 hours to re-write a statement on its website relating to its design rights dispute with Samsung, UK judges have ruled.
Apple logo on building
Apple said it believed the message had been in compliance with the court order

Apple was forced on 18 October to publish a message making it clear that Samsung had not infringed the iPad's registered design.
However Samsung complained the statement Apple had posted did not comply with the court order.
Judges agreed and have told Apple it must be removed within 24 hours.
A new, compliant version must then be posted.
Michael Beloff QC, representing Apple, told judges that the company had thought that it had complied with the court order.
"It's not designed to punish," he said.
"It's not designed to make us grovel. The only purpose must be to dispel commercial uncertainty."
He asked that the company be given 14 days to post the replacement - but the request was firmly denied.
Lord Justice Longmore told Mr Beloff: "We are just amazed that you cannot put the right notice up at the same time as you take the other one down."

The mayor of Amsterdam says he will not ban foreign tourists from using the city's famous cannabis cafes, after months of argument over new drug laws


The mayor of Amsterdam says he will not ban foreign tourists from using the city's famous cannabis cafes, after months of argument over new drug laws.
Protestor lights marijuana joint, Amsterdam 20 April 2012
The move comes after the new government of the Netherlands said it would be up to local authorities whether or not to impose such a ban.
Mayor Eberhard van der Laan said banning the sale of the drug to foreigners could lead to more crime.
Each year, some 1.5 million tourists visit Amsterdam to consume cannabis.
"The 1.5 million tourists will not say 'then no more marijuana', they will swarm all over the city looking for drugs," said Mayor Van der Laan, who has long opposed a ban.
"This would lead to more robberies, quarrels about fake drugs, and no control of the quality of drugs on the market - everything we have worked towards would be lost to misery."
Tourism fears
Amsterdam also relies heavily on tourism, and cannabis users make up about a third of its total visitors.
Under laws introduced by the previous conservative-led Dutch government, a national ban on foreigners using cannabis was due to be rolled out to Amsterdam by the end of this year.
It was intended to curb drug use and prevent drug dealers from operating in the Netherlands, and prevent them from buying drugs to sell abroad.
The move was strongly opposed by cafe owners, who said the law unfairly discriminated against other EU residents, and warned that 90% of their income came from foreign tourists.
There are an estimated 700 coffee shops selling cannabis in the Netherlands.
It is not strictly legal to use cannabis, but its use is tolerated and possession of small amounts was decriminalised in the 1970s.

Elephant 'speaks Korean' with help of his trunk



An Asian elephant called Koshik has astounded scientists with his Korean language skills.
Researchers report that the mammal has learnt to imitate human speech and can say five words in Korean: hello, no, sit down, lie down and good.
The zoo animal places the tip of his trunk into his mouth to transform his natural low rumble into a convincing impression of a human voice.
The study is published in the journal Current Biology.
Koshik's vocal abilities mean that elephants now join a growing list of animals that are able to mimic man, from parrots and mynah birds to more unusual animals such as sea lions or the recently reported case of ahuman-sounding beluga whale.
Meaningful conversation?
The study's lead author Dr Angela Stoeger, from the University of Vienna in Austria, said she first came across Koshik after videos of the elephant, who belongs to Everland Zoo in South Korea, were posted on YouTube.
After making contact with the zoo, she went to South Korea to record the animal so she could study its unusual vocal talent.
Dr Stoeger said: "We asked native Korean speakers, who had never experienced the elephant before, to write down what they understood when we played back recordings from Koshik. check out this link;http://www.bbc.co.uk/news/science-environment-20142858

Jeshi Nigeria linakiuka haki za binadamu

Wanajeshi wa Nigeria wakishika doria

Amnesty international linasema, visa vya watu kupigwa risasi na wanajeshi au kupigwa hadi kufa ni kawaida katika eneo la Kaskazini 

Race to the White House


Race to the White House

Obama49%
Romney49%
Poll of polls, 29 October

President Barack Obama is to resume an election campaign suspended in the aftermath of storm Sandy, which wreaked havoc in the north-eastern US.


Ruined homes in Seaside Heights, New Jersey, 31 October 2012
Mr Obama has planned campaign stops on Thursday in Nevada, Colorado and Wisconsin.
On Wednesday, he toured parts of New Jersey struck by the storm with Republican Governor Chris Christie.
President Obama pledged help for those affected by Sandy as he visited Brigantine, New Jersey
"You guys are in my thoughts and prayers," the president said during a visit to an emergency shelter in Atlantic City. "We are going to be here for the long haul."
More than five million homes and businesses across the north-east still have no electricity. Some utilities are warning it could take seven to 10 days to restore full power.
In the New Jersey city of Hoboken, across the Hudson River from New York City, the National Guard has arrived to evacuate about 20,000 people and distribute meals.
Gov Christie, usually one of Mr Obama's fiercest critics, spoke of his "great working relationship" with the Democratic president.
"I cannot thank the president enough for his personal concern and compassion for the people of our state," said Mr Christie.
Mr Romney held two rallies in Florida on Wednesday, where his campaign said he tried to strike a "positive tone".
Election day is on 6 November, and polls suggest the candidates are running neck and neck.
Affected areas map

BONDIA WA TANZANIA ULINGONI AFGHANISTAN


Afghanistan inaandaa pigano la kwanza la ndondi kuwahi kufanyika nchini humo huku kukiwa na ulinzi mkali sana. Matanzia Said Mbelwa atatoana jasho na muafghani Hamid Rahimi. hapa

TASWIRA NA VIDEO YA WAZIRI WA UCHUKUZI DR HARISON MWAKYEMBE AKIZINDUA USAFIRI WA TRENI KATIKA JIJI LA DAR ES SALAAM

DEREVA WA BODABODA (PIKPIKI) AMETOROKA NA BODABODA YA MWAJIRI WAKE


Pichani ni GODWIN ALLEN UISSO ambaye ametoroka na piki piki ya mwajiri wake.


Bw. Nocodemus Mwasuka ambaye ni mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam akimkabidhi piki piki Bw. Godwin Allen Uisso ambaye alikuwa ni dereva wa piki piki aliyotoroka nayo.

KIJANA KWENYE HIYO PICHA YA KWANZA NA YA PILI NIKIMKABIDHI BODABODA, ANAFAHAMIKA KAMA GODWIN ALLEN UISSO, (Maarufu kama GODI) MKAZI WA TABATA MSIMBAZI (LAKINI KWA SASA AMEHAMA NYUMBA ALIYOKUWA ANAKAA) NA SIMU YAKE HAIPATIKANI TOKA TAREHE 12/10/2012 ILA MARA CHACHE HUWA ANANIBIP NIKIMPIGIA ANAKUWA AMEZIMA SIMU NA HAPATIKANI NA MAJIRANI NA WAPANGAJI WENZAKE WAMEKIRI KUWA ALIKUWA NA TABIA YA UTAPELI… ASILI YAKE NI TARAKEA ROMBO.

PIKIPIKI NILIMKABIDHI TAREHE 15/9/2012 KWA MAKUBALIANO KUWA ALETE HESABU KILA BAADA YA SIKU SABA (MIKUPUO MIWILI ALILETA HESABU LAKINI BAADA YA HAPO NDIO AKAANZA KUPOTEA KWENYE SIMU).

KIJANA HUYO ALIKUWA ANAPAKI BODABODA HIYO MAENEO YA KIGOGO DARAJANI NA KWA SASA HATA PALE GOLINI KWAO HAJAONEKANA.

MAELEZO YA PIKIPIKI NI T-BETTER NAMBA T 935 BUA RANGI NYEKUNDU ... NA NDIO KATOKOMEA NAYO KUSIKOJULIKANA... ANATAFUTWA KWA RB NO.OB/RB/19001/2012

ANAKOPENDA KUSHINDA

1. KIGOGO MWISHO

2. TABATA

3. KIMARA

4. MBAGALA

5. MAGOMENI

NAOMBA YEYOTE ATAKAYE MUONA ATUSAIDIE KUMKAMATA NA KUTOA TAARIFA KITUO CHA POLISI KILICHOPO JIRANI AU PIGA SIMU NAMBA. 0719 575791 begin_of_the_skype_highlighting            0719 575791      end_of_the_skype_highlighting... ZAWADI NONO ITATOLEWA

KIONGOZI WA UPINZANI RWANDA AHUKUMIWA JELA

          

Kiongozi wa upinzani nchini Rwanda Victoire Ingabire amehukumiwa miaka minane gerezani baada ya kupatikana na hatia ya kosa la uhaini
Viongozi wa mashtaka walitaka afungwe maisha jela kwa kutishia usalama wa nchi.
Mahakama imempata na hatia ya kupuuza mauaji ya Kimbari yaliyotokea mwaka 1994.

Friday, 19 October 2012

TAARIFA KAMILI KUHUSU VURUGU ZA ZNZ SASA HIVI NA ASKARI ALIYEUWAWA.



Mpaka sasa hivi hali katika baadhi ya vitongoji visiwani Zanzibar sio shwari pamoja na kwamba serikali imetoa tamko kuwataka wananchi kuendelea na shughuli zao kama kawaida.
Vurugu zilianza toka jana kutokana na kukamatwa kwa kiongozi wa taasisi ya kiislamu, Sheikh Farid Hadi Ahmed ambapo msemaji wa polisi Znz Mohamed Mhina amesema mpaka leo wafuasi wa kikundi cha Uamsho wameendelea na vurugu na uchomaji wa matairi barabarani na kuweka mawe.
Kwenye sentensi nyingine ni kwamba leo ndio imethibitishwa kuuwawa kwa  askari polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia FFU Saidi Abdul-Rahman, ameuwawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo.
Pamoja na watu waliofanya tukio hilo kutofahamika msemaji wa polisi Mhina amesema wanaosadikiwa kufanya hilo tukio ni wafuasi wa kikundi cha Uamsho ambapo mwili wake imepatikana na imefanyiwa uchunguzi kwenye hospitali kuu ya mnazi mmoja.
Mpaka sasa watu 10 wamekamatwa kutokana na fujo hizo vilevile Polisi wanaendelea kutafuta mahali alipo kiongozi wa kikundi cha Uamsho ambae alidaiwa kupotea tangu juzi jioni (jumanne) ambapo alimtuma dereva wake apeleke umeme nyumbani, dereva aliporudi kumfata hakumkuta.

Unaweza kumsikiliza Wakili wa Sheikh Ponda hapo chini…

TAARIFA KAMILI KUHUSU WAUMINI 50 WA DINI YA KIISLAMU KUFIKISHWA MAHAKAMANI LEO DSM.



Jumla ya waumini 50 wa Dini ya Kiislamu, ambao ni wafuasi wa Sheikh ISSA PONDA pamoja na yeye mwenyewe, leo wamefikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu, kujibu kesi ya wizi wa mali na uvamizi wa Ardhi inayowakabili.
Washitakiwa hao 50 kwa pamoja wanakabiliwa na Mashitaka Manne, yakiwemo ya kula njama kwa nia ya kutenda kosa kinyume cha sheria, kuingia kwa nguvu kwa lengo la kutaka kutenda makosa, kumiliki kwa nguvu ardhi ya Kampuni ya AGRI-TANZA, wizi wa matofali 1,500, na kokoto tani 36 vyote vikiwa na thamani ya shilingi milioni 56.6.
Wakili mwandamizi wa Serikali TUMAINI KWEKA, amesema kuwa pamoja na makosa hayo manne, mtuhumiwa namba moja Sheikh ISSA PONDA anakabiliwa na shitaka jingine la Tano, la uchochezi wenye nia ya kutaka kutenda kosa.
Akisoma mashitaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi STEWART SANGA, wa Mahakama ya Haklimu mkazi Kisutu, aliyemuwakilisha Hakimu Mkazi Mfawidhi VICTORIA NONGWA ambaye yupo kwenye Semina, Wakili KWEKA ameitaka mahakama itoe masharti magumu kwa washitakiwa 49, ili watakapotoka wasirejee kwenda kutenda makosa.
Kwa upande wa mshitakiwa wa kwanza Sheikh PONDA, Wakili KWEKA amesema kwamba Mwendesha mashtaka Mkuu wa Serikali DPP ELIEZA FERESHI, ameiandikia mahakama kuitaka kutompatia dhamana mshitakiwa huyo, kutokana na sababu za Kiusalama na Maslahi ya Jamuhuri, jambo ambalo limepingwa na wakili wa washitakiwa JUMA NASSORO, aliyetaka kuainishwa kwa sababu zaidi za kutotaka dhamana hiyo.
Licha ya kupinga agizo hilo la DPP pia Wakili NASSORO ameiomba mahakama, kumlegezea masharti mshitakiwa mwenye umri mkubwa kuliko washitakiwa wote, aliyemtaja kwa jina la ZAIDA YUSUPH mwenye umri wa miaka 100, kutokana na hali yake ya kiafya.
Kabla ya uamuzi wa Hakimu, Wakili KWEKA ameiambia mahakama kuwa haina uwezo kisheria wa kupinga maagizo yaliyotolewa na DPP, hivyo ombi la wakili wa washitakiwa haliwezi kufanyiwa kazi.
Baada ya maelezo ya mawakili hao, Hakimu STEWART SANGA amesema hawezi kusikiliza ombi lolote wala kutoa maamuzi, kutokana na kutokuwepo kwa hakimu mwenye dhamana ya kusikiliza kesi hiyo, na hivyo kuwataka watuhumiwa wote kurudi Rumande mpaka Novemba Mosi, ambapo kesi hiyo itatajwa tena.
Sheikh PONDA aliwasili katika viwanja vya mahakama ya Kisutu majira ya Saa sita na dakika ishirini, akiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi, ambapo kesi ilianza kusomwa na kudumu kwa zaidi ya saa moja, huku ndugu wa washitakiwa wakiwepo nje kusubiri hatma ya ndugu zao.

Wednesday, 3 October 2012

BREAKING NUUUUUUUUZ: AJALI MBAYA IMETOKEA MBALIZI MBEYA MAGARI MAWILI YAMEGONGANA NA KUWAKA MOTO... WATU KUMI WAMEFARIKI DUNIA HAPO HAPO.


Breaking nuuuuuuuuz: Ajali mbaya imetokea mbalizi Mbeya magari mawili yamegongana na kuwaka moto... watu Kumi wamefariki dunia Hapo hapo. Tukio kamili linakuja Punde .. Fuatilia www.mbeyayetu.blogspot.com

MELI MPYA YA KISASA YA AZAM MARINE YENYE UWEZO WA KUBEBA ZAIDI YA WATU 1000 NA MAGARI 200 YAWASILI NCHINI.

 Baadhi ya wakazi wa Zanzibar wakipiga picha Meli hiyo iliyowasili Visiwani Zanzibar leo.
 Meli ya Azam Marine inayoitwa Azam SeaLink 1 ikiwasili katika bandari ya Visawani Zanzibar kwa mara kwanza.
 Mzee Said Bakheresa (mwenye nguo nyeusi) akikagua mazingira ya Meli hiyo baada ya kuwasili Bandari ya Zanzibar leo.
 Sehemu ya Parking yenye uwezo wa kuingiza magari 200.

Muonekano wa ndani wa Lounge ya kumpzikia wasafiri.

Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi Zanzibar

Kampuni ya Azam Marine inayomiliki boti ziendazo kasi hapa nchini, leo imeingiza meli mpya na ya kisasa itakayochukua zaiidi ya abiria 1500 na magari 200.

Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam Marine, Bw. Hussein Mohammed Saidi, amesema leo mjini Zanzibar kuwa meli hiyo ambayo itafanya safari zake kati ya Dar es Salaam, zanzibar na Pemba itatoza nauli nafuu kwa abiria wake.

Amesema meli hiyo ambayo inatarajiwa kuanza safari zake mara baada ya kukamilisha taratibu za mamlaka mbalimbali.

Meli hiyo inayoitwa AZAM SEALINKI ni ya kisasa katika ukanda huu wa Mwambao wa nchi za Kusini na Pembe ya Afrika.

Bw. Hussein amesema Meli hiyo ambayo imetengenezwa nchini Ugiriki na inatayarishiwa eneo maalumu litakalotumika kwa kupakia na kushusha abiria na mizigo yakiwemo magari.

Amesema meli hiyo itasafiri kwa muda wa saa tatu kutoka Dar es salaam na Zanzibar na saa 4 kutoka Zanzibar na Pemba ama saa 7 kutoka dar es salaam na Pemba.

Amesema pamoja na kuwasili kwa Meli hiyo, Kampuni ya Azam pia inatarajia kuleta meli nyingine ya abiiria inayojulikana kama Kilimanjaro namba 4.

Kwa upande wao, baadhi ya wananchi wa Visiwa vya zanzibar wamepongeza ujio wa meli hiyo lakini wakaitaka serikali kuendelea kudhibiti uingizwaji wa meli chakavu na kukuu ili kuepuka uwezekano wa kutokea ajali za mara kwa mara.

Bwana Rajabu Khamisi mkazi wa Pemba na Bi. Rehema Omari wa mjini Zanzibar, wamesema kuna haja ya Serikali kusimamia ukomo wa nauli ili kila mwananchi aweze kusafiri kutoka sehemu moja na nyingine kwani wamesema vipato havilingani.

RICK ROSS WA BONGO KUMPOKEA AIRPORT RICK ROSS WA MAREKAN

                                       Rick Ross Kutoka USA
Rick Ross Ajipange atapokuja Tanzania Tarehe 06 Oct 2012 kukutana na look i like wake....huendi Baba ake alicha mbegu Bongo..lol.
 Rick Ross wa Bongo kumpokea airport Rick Ross wa Marekani, ama kweli duniani wa wili wa wili
Rick Ross wa Bongo huyu hapa

Jinsi Basi la Dar Express Lilivyowaka Moto Njia Panda ya Dar,Arusha,Tanga(Segera)


Basi la  Dar Express limepata ajali ya kuungua moto leo asubuhi katika njia panda ya Dar, Arusha, Tanga (Segera) hakuna mtu aliyejeruhiwa wala kupoteza maisha. Katika ajali hiyo mizigo yote iliteketea kwa moto huo ambapo abiria wengi waliokuwamo kwenye gari hilo walikuwa ni wanafuzi.Picha na Samweli Mikuza

Sunday, 30 September 2012

VURUGU KANISANI: ASKOFU MOKIWA ANUSURIKA KIPIGO KUTOKA KWA WAUMINI, AOKOLEWA NA POLISI

ASKOFU  Mkuu wa Kanisa la Anglikana Tanzania  la  Dk. Valentino  Mkowa leo amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kunusurika kupata kipigo kutoka kwa waumini wake waliokuwa wenye hasira kali.

Vurugu kubwa ziliibuka mara  baada ya kusomwa kwa  tamko lililothibitisha kuwa nyumba ya maaskofu inamtambua  Askofu Canon Kasagara kuwa ni kiongozi wao halali wa kanisa la Anglikana la watakatifu wote Jimbo  la Ziwa Rukwa mjini Sumbawanga.

Katibu mkuu wa Anglikana Dk, Dickson Chilongani ndiye aliyesoma tamko hilo mara baada ya kumalizika kwa ibada iliyoongozwa na Askofu Mkuu Dk. Mokiwa.

Akisoma tamko hilo Katibu Mkuu alisema kuwa sehemu ya hoja za msingi kamati ya usimamizi wa kanisa hilo zilidai kuwa uchaguzi uliomweka madarakani Askofu Kasagara uligubikwa na rushwa,si za kweli na  nyumba ya maaskofu imeshindwa kuthibitisha hilo hivyo Kasagara ni askofu wao halali.

Kutokana na kauli hiyo waumini hao, walianza kupiga kelele ya kupinga maelezo hayo hali iliyosababisha mjumbe  wa Kamati ya kusimamia kanisa hilo Flugence Lusunzu aliposhika kinasa sauti na kueleza kuwa wanao ushahidi wa kutosha kuwa rushwa ilitumika kwenye kinyang’anyiro cha  uchaguzi huo uliofanyika zaidi ya miaka miwili iliyopita.

Alidai kuwa uamuzi wa nyumba ya maaskofu haukuwapa fursa ya kusikiliza upande wa walalamikaji ili hali ushahidi upo wazi, kutokana kauli hiyo zilianza fujo zilisababisha askofu Mokiwa kutolewa lugha chafu, kuvuliwa kufia yake ya kiaskofu, huku wengine warusha viti ambavyo alivikwepa hado alipoondolewa akiwa chini ya polisi waliokuwa wamevalia kiraia.

Hali hiyo iliharibu amani iliyokuwa imetawala ndani ya Kanisa hilo ambapo uligeuka kuwa uwanja wa vita huku waumini wakisikika wakidai kuwa ni heri kanisa hilo lifungwe kuliko Askofu Kasagara kuliongoza.

Awali tangu nyakati za asubuhi, polisi waliovaa kiraia walitanda katika viunga vya kanisa hilo ambapo Askofu Mokiwa aliwasili na kulakiwa vizuri na waumini wake waliokuwa wakishangilia kwa nyimbo na mapambio.

Hata hivyo tayari waumini wa Kanisa hilo walionya kwamba askofu Kasagara asikanyage kwenye eneo hilo, kwani kufanya hivyo kunge hatarisha amani onyo ambalo upande wa askofu Kasagara walitii hivyo askofu huyo mwenye makazi yake wilayani Mpanda alibaki katika nyumba moja ya kulala wageni alikokuwa amefikia.

Mmoja wa waumini  Julius Michael alisema kwa kuwa waumini wa Jimbo la Rukwa hawamtaki askofu Kasagara hakuna sababu ya kuwalazimishwa lakini  nyumba ya maaskofu inapaswa kuangalia uwezekano wa kuligawa jimbo hilo.

Tayari Serikali imegawa mkoa wa Rukwa na kuzaa ule wa Katavi sasa hakuna umuhimu wa kuwalazimisha waumini wampokee mtu wasiyemtaka nyumba ya maaskofu waanzishe jimbo katika mkoa huo mpya na aongoze Kasagara.

 Alisema iwapo watatumia nguvu kumuweka Askofu huyo Rukwa haitasaidia kitu kwani hawezi kuwaongoza watu wasiotaka kushirikiana nae.

Mgogoro katika Kanisa hilo umedumu kwa zaidi ya miaka miwili sasa ambapo siku za nyuma waumini hao  walimzuia  Askofu  Mkuu,  Dk  Valentino  Mkowa  kumsimika  Askofu  huyo  na  badala  yake  alisikimkwa  tarehe 16, Juni mwaka jana   Mjini  Mpanda.

Kutokana na kujitokeza kwa mgogoro huo, ilifunguliwa  kesi mahakamani ya Hakimu Mkazi Sumbawanga na waumini wa anglikana, Fulgence Rusunzu na Rojas Bendera  na wenzao 191 yenye  namba 11/2011 wakipinga kuchaguliwa kwa askofu Kasagala kuwa kiongozi wa Dayosisi hiyo.
 Mmoja wa waumini wa kanisa la Anglikana la watakatifu wote la mjini Sumbawanga akiwa na jazba wakati wa vurugu zilizoibuka jana mara baada ya kutolewa uamuzi wa nyumba ya maaskofu wa kuridhia  askofu Mathayo Kasagara kuwa kiongozi wao ambapo vurugu kubwa zilizuka na kusababisha askofu Mkuu wa kanisa hilo Dk Mokiwa kuondolewa akiwa chini ya ulizi wa polisi. picha na Mussa Mwangoka
  Waumini wa Kanisa la Anglikana la watakatifu wote mjini Sumbawanga jana wakipiga kelele kupinga uamuzi wa nyumba ya maaskofu wa kuridhia  askofu Mathayo Kasagara kuwa kiongozi wao ambapo vurugu kubwa zilizuka na kusababisha askofu Mkuu wa kanisa hilo Dk Mokiwa kuondolewa akiwa chini ya ulizi wa polisi. PIcha na Mussa Mwangoka
Askofu Mkuu wa Angikana Tanzania,la Dk. Valentino  Mkowa aliyevuliwa kofia ya kiaskofu akiwa chini ya ulinzi wa polisi waliokuwa wamevalia kiraia wakimtoa nje ya Kanisa la Anglikana la watakatifu wote mjini Sumbawanga baada ya kuzuka kwa vuguru kubwa jana. Picha na Mussa Mwangoka