Friday, 24 February 2012

ALIEANDIKA WIMBO MPYA WA CHRIS BROWN & RIHANNA NDIO HUYU, ISOME STORI ALIYOITOA KUHUSU WAWILI HAO


Baada ya single ya Rihanna aliyomshirikisha Chris Brown iitwayo Birthday cake rmx kuanza kupigwa kwenye radio duniani toka ilipotoka wiki hii, Mwandishi/Producer/mwimbaji THE DREAM ambae amehusika kuiandika hiyo track ameamua kuzungumza ukweli.
Amekiri kwa kusema idea ya kumuweka Chris Brown kwenye hiyo track ilitoka kwa Rihanna mwenyewe na anakumbuka yeye, yani The Dream alikua yuko barabarani anaendesha gari huko Miami Marekani alafu Rihanna akampigia simu, akamwambia “nadhani nitamshirikisha Chris kwenye hiyo track, The DREAM  akajibu sijui ni Chris gani unamuongelea, lakini poa sina tatizo na ulichosema…. baada ya hapo Rihanna hakusema kitu na ndio ikaishia hivyo mpaka The DREAM akaja kufaham kwamba ni Chris Brown ndio kapewa mzigo.
Kwa kumalizia The DREAM amesema mbali na kuwa wanafanya kazi pamoja na Rihanna, mwimbaji huyo pia ni rafiki yake wa karibu ndio maana ni rahisi kushirikiana au kuhusisha mawazo kama hayo, ambapo kuhusu mshangao wa wengi kwamba imekuaje Chris Brown na Rihanna wakarudi tena kufanya kolabo wakati kulitokea ugomvi mkubwa kati yao 2009, amesema “tunatakiwa kujifunza kusamehe, na tukisamehe inatakiwa iwe kweli kutoka moyoni sio mdomoni tu”

No comments:

Post a Comment