Monday, 27 February 2012

MUGABE ALIVYOSHEREHEKEA BIRTHDAY YAKE!

Matawi ya chama cha ZANU PF cha Rais Mugabe, yalichanga kugharimia sherehe hizo ambazo pia zilikuwa na mashindano ya warembo na mechi ya mpira ambapo rais huyo aliwaambia wafuasi wake kwamba wale wanaopinga msimamo wake dhidi ya wapenzi wa jinsia moja na ndoa kati yao, wapotelee mbali.
Sherehe za kuadhimisha siku ya kuzaliwa ya Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe kutimiza umri wa miaka 88, zimefanywa katika mji wa Mutare, mashariki mwa nchi hiyo ambapo maelfu ya watu wamehudhuria.
Rais huyo pia alikanusha kuwa ni mgonjwa, ikiwa ni siku kadhaa baada ya kusema atakazana kama kigongo na bado  anaweza kuongoza nchi huku Umri wake pamoja na taarifa kuwa anaugua saratani ya kibofu, zimeshawishi kwamba chama hicho kinahitaji kiongozi mwingine japo chama chake kimemuunga mkono agombee tena urais mwaka huu.

No comments:

Post a Comment