Wednesday, 22 February 2012


WAZIRI WA NCHI OFISI YA MAKAMU WA MUUNGANO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO ZANZIBAR

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan akionyeshwa kito kinachotengeneza Lulu ambayo hufanywa Pete na Katibu wa Kampuni ya Ukweli ni Njia Safi Bi Safia Hashim alipotembelea kikundi cha akina mama cha Bweleo Wilaya ya Magharibi Unguja wakati wa Ziara yake ya kuangalia Miradi ya Maendeleo ya [TASAF] inafadhiliwa na Serikali ya Muungano.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Muugano Samia Suluhu Hassan akipata Maelezo kwa Bi Mwajuma Mwinyi kuhusu Matumizi ya Mwani wa Baharini ambao wanatengenezea Sabuni ya Kuogea na huweka Unyevunyevu kwenye ngozi kuifanya nyororo wakati wa Ziara yake ya kutembelea Miradi ya Maendeleo inayofadhiliwa na Serikali ya Muugano huko Bweleo Wilaya ya Magharibi Mjini Unguja[Picha na Ali Meja]


======== =====    =====================  ==============
 Na Ali Issa Maelezo.

Mamlaka ya kusimamia uvuvi wa bahari kuu Tanzania imeimba serikali ya jamuhuri ya muungano Tanzania na ile ya Zanzibar  kuiridhia  sheria ilopo na kuipitisha  iliweze kufanya kazi zake vizuri na kutekeleza vyema kazi zake  mamla.

Hayo yamesemwa leo huko kinazini katika jengo la ZSTC Zanzibar  na   Mkurugenzi wa mamlaka hiyo Geofrey Frank Nanyaro  wakati wamazungumzo kati ya malaka na Ofisi inayo shughulikia masuala ya muungano Tanzania mbele ya waziri  Samia Suluhu Hasani aliofika hapo akiwa ziarani kutembelea maeneo hayo .

Amesema malaka ya kusimamia bahari kuu ni taasisi ilio undwa kupitia sheria ya malaka ya kusimamia uvuvi kwenye eneo la ukanda wa kiuchumi EEZ ya mwaka 1998 ambayo ilifanyiwa marekebisho kupitia sheria namba nne ya mwaka 2009 sheria  ambayo ilishirikishA Pande zote mbili za muungano  na badalayake ikapelekwa baraza la mawaziri na  kukubaliwa lakini upande wa pili wa  baraza la wawakilishi hadisasa bado kuridhia sheria hiyo .

Amesema kuchelewa kuridhia sheria hiyo nikufanya kazi katika mazingira ambayo hayaendani  na kazi kisheria na  kuyafanya kuwa mazingira  magumu katika utekelezaji wakazi zake kitalamu  .

“Nivigumu kutekeleza kazizetu kitaalamu kwani sheria ndio inayo muongoza mtu kufanyakazi vyema hivyo  ikawa sheria haijaridhiwa itakuwaje juu yakusimamia baharikuu ambao wanao kuja kuvua wanafahamu kilakitu .”alisema Geofrey .  Aidha mkurugenzi huyo alisema kuwa kuchelewa kuridhiwa kwasheria hiyo kuna wakosesha frusa wataalamu wao hata kupata  mafao yao kimsingi  kamavile mishahara nahatimae kupata posho tu.  Amesema halihiyo haipendezi kwani inaleta uchovu katka uwajibikaji na misingi boa ya kazi .

Nae mtaalamu wamtambo unao toa ripoti za meli za kigeni zinazo ingia nchini Damian Boniface Chando amesema kua Malaka hiyo hivisasa inauwezo wa kugundua meli zinazo ingia  na kutoka kaita ukanda wa baharikuu  zinazo vuasamaki  kinyemela kwa kutumia mtambo wa Vessl monitoring system ambao wanao na  unafanyakazi muda wote.

Aidha alisema kuwa mtambo huo unaweza usifanye kazi iwapo mabaharia watafanya uharamia kwa kuzima kifaa   kiitwacho kwa kitaalamu transimitter na wao wasiweze kundua kama samaki wao wanavuliwa kwa kuibiwa. “Ni vizuri kujipanga kua na doria kwani mtambo huu hautoshi pekeyake iwapo mabaharia watafanya uharamia bila  ya  kuomba kibali na kuzima mitamboyao’alisema Boniface  . 

Nae waziri samia alisema wanazichukuwa changamoto zilopo na kwenda kuzifanyiakazi, lakini alisema kua  wakati umefika kwa viongozi kuwa wa wazi na wakweli wanapokuwa katika vikao  na kutekeleza yale wanayo yasema,Amesema katika ziara yake amejifunza    mengi ambayo alikuwa hayajui na sasa anaelewa na atayapeleka munamo husika na kufanyiwa kazi.

Wazirihuyo alitembelea mamlaka ya Uvuvi wa Bahari kuu Fumba Maradi wa MACEP Bweleo  kuangalia madawati yalio na TASAF skuli ya kombeni pamoja na mradi wa kinamama wakutengeneza sabuniza kuogea kwamalighafi ya mwani napete za luu kwamalighafi ya kombe za baharini. 

BENKI YA NBC YAJITOSA KUDHAMINI GOFU LA WANAWAKE NCHINI

Meneja Udhamini na Matukio wa NBC, Bi. Rachel Remona Kimambo (wa pili kushoto) akikabidhi mfani wa hundi ya shs milioni kwa Nahodha wa Kitengo cha Gofu ya Wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam,Vivienne Mwaulambo kusaidia mashindano yao yanayotarajiwa kufanyika Jumapili ijayo katika klabu hiyo jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni maofisa wa NBC na viongozi wa kitengo hicho cha gofu.
Nahodha wa Kitengo cha Gofu ya Wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam, Vivienne Mwaulambo (kushoto) akizungumza kabla ya kupokea msaada msaada huo kutoka benki ya NBC. Katikati ni Meneja Udhamini na Matukio wa NBC, Bi. Rachel Remona Kimambo na kulia ni Katibu wa kitengo, Joyce Svarva.
Maofisa wa NBC pamoja na wa Kitengo cha Gofu ya Wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam wakipiga picha ya pamoja katika hafla hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Nahodha wa Kitengo cha Gofu ya Wanawake cha Klabu ya Gymkhana Dar es Salaam, Vivienne Mwaulambo (wa pili kushoto) akiwa na baadhi ya maofisa wa NBC baada ya kupokea msaada msaada huo kutoka benki ya NBC.Kutoka kushoto ni, Arden Kitomari, Meneja Chapa na Matangazo, Eddie Mhina; Mshauri wa Mawasiliano na Meneja Udhamini na Matukio wa NBC,Bi. Rachel Remona Kimambo.

DK. NAGU AKUTANA NA UJUMBE WA WAWAKILISHI WA UCHUMI NA BIASHARA KUTOKA CHINA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akiongea jambo na aliyekuwa Mwakilishi Mkuu wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania Zhao Zhongqiu leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Zhongqiu alimtembelea waziri huyo kwa ajili ya kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akisalimiana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania Lin Zhiyong leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Zhiyong anachukua nafasi ya Zhao Zhongqiu ambaye amemaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk.Mary Nagu akiongea na ujumbe wa wawakilishi wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam . Ujumbe huo uliongelea mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya Tanzania na China.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk.Mary Nagu (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania walipomtembelea leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Lin Zhiyong ambaye ni Mwalikishi mpya na kulia ni Zhao Zhongqiu ambaye amemaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.Picha na Anna Nkinda - Maelezo.

No comments:

Post a Comment