Hii nafasi nimempa staa wa single ya Nai Nai, Ommy Dimpoz ambae juzi alitangaza kwenye millardayo.com kwamba hawezi kutoa single nyingine mpya kwa sasa kwa sababu nai nai bado inafanya vizuri, huku ikiwa ndio ya kwanza kwenye 20 kali za Clouds Fm.
Stori aliyonayo leo ambayo imenifanya nimpe hii nafasi, ni kitendo chake cha kukubali kutaja pesa anayolipwa kwenye show moja, yani akisimama tu kwenye stage, ujue tayari ameshavuta huo mkwanja.
Ommy amesema sasa hivi ameshapiga showz zisizopungua 15 toka aitoa single ya Nai Nai mwishoni mwa mwaka 2011 na show yake moja kwa Dar es salaam analipwa milioni mbili, kwa mkoani ndio milioni tatu.

No comments:
Post a Comment